Tunafurahi kutembelewa na wenzetu wa Tasnia ya uigizaji kutoka Dar es salaam hapa mkoani Iringa kifupi ni jambo jema na la kujenga mahusiano bora baina ya wasanii.
Tunapenda kuwashukuru kwa sababu zifuatazo
Moja tunajenga mahusiano ya kutambuana baina ya wasanii,kupima uwezo wetu pia.
Pili kupata uzoef wa nini wenzetu mnafaya nasi kujaribu kutoka hatua tuliopo sasa kwenda nyingine angalau tupate kuwa katika level wenzetu mpo.
Pamoja na kuwashukuru kwa hilo basi tuombe uwaminifu katika hilo maana tayari Iringa tulisha umwa na nyoka kwa mfumo na utaratibu huo.
Ni kweli kabisa Sanaa tunaipenda lakini msitumie kigezo cha mapenz yetu ya Sanaa kuibia.Kwa pamoja tutajenga na kuiendeleza sanaaa
No comments:
Post a Comment