Saturday, 6 September 2014

producer benny ashilikiana na khamis nurdin kuiua vipaji vya wasanii wa iringa kupitia studio george rec iliyopo wiloles wakiwa ndani ya miale sanaa group kama unajiona unakipaji wasaliana na benny kwa namba hii 0769 116165 au khamis nurdin 0715 698582




Wednesday, 23 April 2014

ETI HAWA WAREMBO WANADAI WASHAWAHI...........NA ALI K

Ali kiba ni mmoja wa wanamuziki walio kimya sana kwenye upande wa kuongelea mambo yake binafsi, haswa kimahusiano, au hata kujitangaza kumiliki kitu kingine chochote cha thamani kama ilivyo desturi ya wasanii wengi hapa town baada tu ya kupata umaarufu, ila siri hufichuka haswa pale kwa warembo hawa wanapoamua kumwaga mpunga ndipo hapo unapoanza kujua yaliyo chini ya kapeti.Hawa ni warembo waliowahi kukiri kuwa walishawahi kuwa na mahusiano na Celeb huyu mkongwe sana kwenye anga za muziki huu wa Bongo Fleva.
 collagbhveMapenzi ya hawa wawili inasemekana yalianza enzi hizo ambapo wawili hao walikuwa bado hawana majina kabisa hapa town, kila mmoja wao akiwa yupo kwenye hustle zakutoka kila mmoja akiwa natetea fani yake, ila kwa bahati nzuri AliKiba akaanza kupata umaarufu kuitia muziki hata kabla ya Wolper kuanza ku-make headlines kupitia filamu, akiwa kama muigizaji.

“Ni kitambo kidogo sana wote hatukuwa star lakini mwenzangu alifanikiwa kuchomoka,lakini Ali ndiye aliyeniingiza kwenye ulimwengu wa Mapenzi” alifunguka Wolper,
“Ali akawa star,alipokwenda nje nikasikia wanawake wanamshobokea,sasa mimi sikutaka karaha nikakaa pembeni,lakini jamaa ni mtu poa sana na tukikutana tuanasalimiana freshi kabisa” alimalizia akizungumzia sababu zilizomfanya aachane na Kiba wakati huo.

Lulu Michael.
cohllage
haikujulikana mapema kama inavyotokea kwa watu maarufu wengi hapa town, ila mahusiano yao yalianza huko kitabo sana, baina ya Lulu na Ali Kiba, ila mwisho wa siku Lulu aliamua kumwaga mpunga hadharani kufunguka juu ya mahusiano yao.

“Duh! Umenikumbusha mbali sana. Nilishasahau kabisa kama niliwahi kutoka naye. Pamoja na kwamba ni kweli alikuwa mtu wangu, lakini kwa sasa moyo wangu hautaki kusikia kingine zaidi ya Bieber na namuonea wivu sana Selena Gomez (mpenzi wa Bieber).”

ila hakutaka kuzungumzia sababu za kuachana naye, nakusea ilikuwa tu sababu zake binafsi kwa sababu mapenzi yana taba moja kuwa ukiyag’ngania hasa pale ambapo hauenjoy mwisho wake ni kuumizana tu, alimalizia lulu kuelezea safari yake ya mapenzi, na hadi hivi sasa anakiri kuwa bado yupo

Wednesday, 16 April 2014

MAONI YA SHEKH SHARRIF HAMAD KUHUSU MUUNGANO MH....!


  Hammad ambaye kwa siku za karibun amekuwa mmiliki wa vichwa vya habari kutokana na ripoti mbalimbali ambazo zimekua zikimnukuu kwa kudai kutozitaka serikali mbili lakini leo April 15 2014 amezungumza kwenye maonyesho ya miaka 50 ya muungano ya kuzitoa hizi kauli zifuatazo.
1. ‘Pamoja na milima na mabonde, muungano huu umedumu miaka 50, nchi nyingine zilishindwa, lazima tufanye tathmini hasa ya muungano wetu, lazima vijana waelimishwe vp muungano uliundwa, tulianzia vipi’
2.‘Ukitaka upate maenedeleo, yatambue mafanikio yako lakini pia usisahau matatizo yako, ni ni moja.. kufanya vizuri, Sidhani katika Tanzania kama kuna watu hawataki muungano, na kama wapo ni wachache, muungano uendelee ndio la msingi’
3. ‘Sio dhambi watu kuwa na fikra tofauti, sio dhambi hata kidogo kwa sababu hatuwezi wote kuwa na fikra aina moja, Wanaotaka serikali moja wasibezwe, mbili wasibezwe, wanaotaka tatu na serikali ya mkataba wasikilizwe pia’
4. ‘Wako wanaoamini kwamba matatizo ya muungano yako kwenye muundo, tuwasikilize wana hoja gani, Mwaka 1963 Malaysia na Tanganyika maendeleo ya sehemu zote hizi yalikua sawa, mwaka 2014 tujiulize, changamoto kwetu ni vipi tutakua na muungano utakaokua ni chachu ya maendeleo ya haraka, mambo ya 74 ni tofauti na 2014′
5. ‘Tuwe makini sana, sote ni wa nchi moja, tujiepushe na kikundi chochote kuona wao wana haki zaidi, Watanzania wote sawa, wajumbe wa bunge maalum waangalie maslahi ya nchi, muungano huu ni wa nchi 2 zilizokua dola huru na kuungana kwa hiari’
6. ‘Tupate katiba ambayo itaondoa migogoro, kero iwe ni historia… hili swala lisiwepo tena, tusiende kwenye maamuzi ya harahaharaka tukasema serikali mbili au tatu bila kuangalia athari zake, katiba ya Znz inasema ni miongoni mwa nchi mbili za muungano, ya Muungano inasema Tz ni nchi moja, huo ni mgogoro’
7. ‘Nadhani Warioba walivyopendekezwa waliona hisia za Znz zilivyo, tunataka katiba itakayotambua usawa wa nchi mbili, hakuwezi kuwa na katiba ambayo itamridhisha kila mtu lakini angalau wengi wao waridhike’

Mbunge wa Mbeya mjini amwaga cheche bungeni jana

"Mwigulu Nchemba anataka Serikali moja, lakini anaogopa kusema"........... "Mhe.Mwenyekiti, kwanza naunga mkono Serikali tatu kama zilivyoletwa kwetu na TUME ya Katiba ya Jaji Warioba, kwa hiyo tunaunga mkono maoni Wananchi. Aliyeuharibu huu mchakato ni RAIS aliyekuja kueleza msimamo wa Chama chake badala ya kuzindua Bunge. Hiki ni Kipindi cha Kwaresma, acheni unafiki, tumeharibu Pesa nyingi. CCM wameishiwa hoja, wameanzisha mkakati wa kuzomea. MWIGU...LU anataka Serikali moja, lakini anaogopa kusema. Tupo kwenye nafasi nzuri sana ya kulijadili Swala hili, la sivyo, tutalijadili kwa kulazimishwa. Leo LUKUVI anatutishia uwepo wa Serikali tatu, JESHI litaitawala Nchi! Mbona Rais wetu alikuwa Mwanajeshi na anatuongoza?...Wanajeshi ni Ndugu zetu, wakitawala kuna tatizo gani?... Unapopimwa Malaria au Ukimwi, Sample ya Damu inatolewa kidoleni, na sio lita tano ili kujua ngoma imekaaje mwilini! acheni kutuzingua kwamba waliohojiwa na TUME ya Warioba ni wachache". amesema Mhe.Sugu.

Thursday, 10 April 2014

Tuesday, 8 April 2014

WE..MWANAUME FANYA HAYA KAMA UNATAKA KUEPUKA KUCHUNWA NA MADEMU

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhis4Liy1yfJkaw0imNQwOzzs_QontxC-ZL4WZ4uXKQF_kmrymLpTQT703h10rVFtwxjE-2HOn4nDKpiRBpu6vEUTfvf8t3eit5bH_9znU_tYSm51I0Xy-dDEMy80LLWofEa6373ddFBwM/s1600/aa-couple-laying-in-bed.jpgNaongea na wale ambao tayari wamesha jitegemea kimaisha, ambao hawaishi na wazazi wao, wanaokumbana na mkono wa Mama/Baba mwenye nyumba kila baada ya miezi sita mitatu au mwaka..
Wanaoishi ki-bachelor lakini wana wapenzi.
Katika hii movie ya ki-bachelor tunakumbana na mengi sana,,kuna wanaogeuza ma girl friend zao kuwafanya kama mke,,tabia ya aina hii imepelekea na wao kugeuzwa kama waume,,hapa unakuta kila kitu girlfriend anakutegemea wewe akipata kashida kidogo ooohh baby nataka hela..

Mazingira ya kuchunwa tunayatengeneza wenyewe usianze kumhisi binti wawatu ni mchwa,,jichunguze kwanza na wewe kinachofanya akunyoshee mkono.
Ukiweza kuyamudu mambo yaha hakika hautayachukia maisha ya ki-bachelor na kumgeuza girl friend kuwa mke, na yeye pia atashindwa kupata ujasiri wa kukutegemea kiasi fulani labda tu kama nitabia yake..

1. Kujipikia
2. Kufua
3. Usafi wa vyombo.
4. Usafi wa chumba.


Ukiweza kukabiliana na hayo pasipo kutegemea msaada kutoka kwa girl wako utayafurahia sana maisha ya ki-bachelor,,na swala la kuoa kwako utaliamua kwa wakati muafaka, ila sio kwa kuwa unahitaji msaidizi.

Ebu fikiria labda girlfriend wako anakuja kukusalimia siku ya mapumziko, anakuta chumba chako umesafisha vizuri vyombo viko katika mpangilio mzuri,,umefua nguo zako na mashuka,,huku na huku haujachoka kuna akiba ya mchele,,unawasha kajiko kako unapikia wali na unaandaa mboga yani kila kitu unaweka sawa kisha unapakua kwenye hotpot yako, basi akija mnakula kama atapenda,,baada ya chakula mnaendelea na mambo yenu,,kusanya vyombo vyako akiondoka unaviosha.

Kumbuka kufanya hivyo hakuondoi uan
aume wako,,jifunze kudhamini vitu vyako girlfriend hajawahi kukununua hata kijiko vyote umenunua kwa pesa yako,,ulio itolea jasho kwa kugombania daladala asubuhi uwahi kazini.

Hapo unajaribu kutengeneza mazingira ya kumfanya asijihisi unamtegemea sana zaidi ya kitu kimoja tu nadhani unakijua kwa wale mabachelor ambao mnamiliki kiwanja cha fundi selemara chumbani kwako.

Kama bachelor mwenye akili zako timamu lazima uishi kwa malengo ukijua kesho na wewe utakuwa na familia itaishi vipi kama ukiendekeza kuhonga katika ubachelor wako.

Ishi na mwanamke kwa kanuni kama unavyo fanya hesabu,,baada ya hayo kinachofuatia hakikisha unatumia kiasi kidogo sana cha pesa kumnunulia vitu vidogo vidogo ambavyo havina gharama,,ili mkusahaulisha kiasi fulani auone uwepo wako.

Ila kama wewe sio muoga kama mimi basi unamkazia kabisa,,maana demu nae akishajua unapenda pochi manyoya yake basi atakubabaishia,,,usiwe mtumwa wa pochi manyoya.

Kwa style hiyo binti unasababu ya kumtegemea boy wako???

Na wewe bachelor mwenzangu hapo bado unayo sababu ya kugeuzwa kitega

uchumi?????